Add parallel Print Page Options

Yesu Akiwa Mbele ya Viongozi wa Kidini

(Mt 26:59-66; Mk 14:55-64; Yh 18:19-24)

66 Alfajiri, viongozi wazee wa watu, viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikusanyika. Walimpeleka Yesu kwenye baraza lao kuu. 67 Wakamwambia, “Tuambie ikiwa wewe ni Masihi.”

Yesu akawaambia, “Hamtaniamini ikiwa nitawaambia kuwa mimi ni Masihi. 68 Na ikiwa nitawauliza swali, hakika mtakataa kunijibu. 69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu atakaa upande wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”

70 Wote wakasema, “Kwa hiyo wewe ni Mwana wa Mungu?” Akawajibu, “Mnaweza kusema kuwa mimi ni Mwana wa Mungu.”

71 Wakasema, “Je, tunahitaji mashahidi wengine zaidi? Sote tumesikia alichosema yeye mwenyewe!”

Read full chapter